Wednesday, 11 June 2014

List Wanaoongoza kufunga mabao Mengi kombe la dunia,Ronaldo anaweza kupitwa iwapo Klose akifunga mawili tu

Ronaldo de Lima
Tokea kombe la dunia la mwaka  2006, rekodi ya Ronaldo De Lima ya kufunga mabao 15 katika mashindano yote ya kombe la dunia imebaki kuwa historia ila kwa mwaka huu inaweza kuvunjwa.
Ronaldo alicheza kombe la dunia miaka ya  1998, 2002 na  2006.
Sport4lifetz inakuletea kumi bora ya wachezaji waliofunga mabao mengi zaidi,Anayemfuata kwa karibu ana mabao  14 , ni Miroslav Klose mwenye miaka 36 wa Ujerumani sambamba na mjerumani mwenzake ambaye hachezi soka kwa sasa Gerd Muller,.
   Mchezaji/Nchi     Mabao   
Ronaldo-Brazil 15
Miroslav Klose-Ujerumani 14 
Gerd Muller-Ujerumani 14 
 Just Fontaine-Ufaransa 13
 Pele-Brazil 12 
 Sandor Kocsis-Hungary 11 
 Jurgen Klinsmann-Ujerumani 11 
 Helmut Rahn-Ujerumani 10 
 Gary Lineker-uingereza 10 
 Gabriel Batistuta-Argentina 10 
 Muller aliyecheza soka miaka ya 1970 na  1974 na kufunga bao kwa wastani wa 1.08 kwa mchezo moja wa kombe la dunia.

Nyota wa zamani wa Ufaransa  aliyecheza soka miaka ya 1958 Just Fontaine - amefunga mabao  13 .

Akiwa na mabao 12 katika mashindano nne ya kombe la dunia  kuanzia  1958 na 1970, gwiji wa Brazil  Pele ni nyota kwenye nchi yake akiwa na mabao hayo na kubeba kombe mara 3

Wachezaji wawili wamefunga mabao  11 kila moja , gwiji wa Hungary  Sandor Kocsis na Mjerumani   Jurgen Klinsmann.
Kumi bora inafungwa na Mjerumani  , Helmut Rahn, mwaka wa 1954 na 1958, mshambuliaji wa zamani wa Uingereza  Gary Lineker pamoja na Muarjentina, Gabriel Batistuta.

Iwapo mwaka huu David Villa wa Hispania  (mabao 8) au  Diego Forlan wa Uruguay (mabao ) wakifunga mabao mengi mwaka huu kule Brazil wanaweza wakaingia kwenye list.
Taarifa hizi ni kwa mujibu wa Sports4lifetz kushirikiana na Goal.com

0 comments:

Post a Comment