Kaka amfuata David Villa kule Marekani.
Kiungo wa klabu ya AC Milan Ricardo Izecson dos Santos Leite maarufu Kaka amefikia mahali pazuri katika maongezi na klabu ya Orlando City ambapo atajiunga hapo January 2015, katika ligi ya Marekani, MLS imeeleza taarifa ya klabu hiyo.Mchezaji huyo mwenye miaka 32 alijiunga tena na klabu ya Milan baada ya kuitumikia klabu ya Real Madrid miaka minne pasipo mafanikio.
Kaka ambaye mapema alizungumza na klabu hiyo kwa sasa mambo yanakaribia kumalizika.
“Klabu ya Orlando City imefikia hatua ya mwisho na Kaka. kwa sasa tumefika makubaliano binafsi,
Kaka atajiunga na Orlando City SC hapo January 2015 kabla ya kuanza kwa MLS." taarifa ya klabu ya Orlando City.
Mbrazil huyo amaefunga mabao 29 katika michezo 87 kwa upande wa selecao ameshinda taji la ligi ya mabingwa ulaya akiwa na Milan mwaka 2007 na ameshinda taji la Serie A na La liga akiwa na Madrid.
Kaka siku za hivi karibuni alikaririwa akisema kuwa angependelea zaidui kucheza Marekani iwapo ataondoka Milan.
Iwapo Kaka atafanikiwa kujiunga na Orlando City, atakuwa mchezaji wa pili mwenye jina kubwa duniani kujiunga na ligi ya MLS kufuatia David Villa kujiunga na New York akitokea Athletico Madrid.
0 comments:
Post a Comment