Kipa Friedel asaini Spurs,sasa kuvunja rekodi huko Uingereza.
Klabu ya Tottenham Hotspur imemuongezea Mkataba wa Mwaka Mmoja Kipa wao Brad Friedel na sasa yupo njiani kuvunja Rekodi ya Mchezaji mwenye Umri mkubwa kuchezea Ligi Kuu Uingereza.
Friedel, mwenye Miaka 43, ataivunja
Rekodi inayoshikiliwa na John Burridge wa Manchester City ambaye Mwezi
Mei 1995 alicheza dhidi ya Queens Park Rangers akiwa na Umri wa Miaka 43
na Siku 162.
Kipa huyo Mmarekani alihamia Tottenham
Julai 2011 kutoka Aston Villa kwa Uhamisho Huru na amekuwa akitumika
kama chaguo la pili kwa Hugo Lloris ambae ni Kipa Nambari moja wa Ufaransa.
Msimu uliopita, Brad Friedel alidakia
Mechi moja ya Ligi na Msimu huu mpya unaokuja Spurs inataka kumtumia
hasa kama Balozi wao huko Marekani lakini anaweza kuja kuitwa ili adake
na hivyo anaweza kuivunja Rekodi ya Mchezaji Mzee kwenye Ligi Kuu Uingereza.
Friedel amecheza Ligi Kuu Uingereza kwa Miaka 17 akidakia Klabu za Liverpool, Blackburn Rovers na Aston Villa kabla kuhamia Spurs ambako amecheza mara 67.
Pia ameidakia Nchi yake ya Marekani mara 82 na kucheza Fainali za Kombe la Dunia mara mbili.
0 comments:
Post a Comment