Monday, 30 June 2014

Klose na Rekodi ya mabao kwa timu za Afrika,leo ataweka rekodi mbele ya Algeria? Ronaldo alifanya hivyo.

Baada ya Mchezaji  Miroslav Klose wa Ujerumani kufanikiwa kusawazisha rekodi iliyokuwa inashikiliwa na nyota wa zamani wa Brazil  Ronaldo de Lima ya kufunga mabao 15 katika fainali za kombe la dunia,leo wengi wanasubiri iwapo atavunja rekodi hiyo.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka  36 ambaye mwaka huu anacheza fainali zake za nne alifunga bao lake la 15 la mashindano ya kombe la dunia katika dakika ya  71 na ni bao lake la  69 katika mashindano ya kimataifa,Ujerumani ilipocheza na Ghana.

Klose  mfungaji bora wa kombe la dunia mwaka 2006    akiwa na mabao 5  alimaliza akiwa wa pili  mwaka  2002 akifunga mabao 5 pia na kule Afrika ya kusini mwaka 2010.
Akifunga bao katika mchezo wao dhidi ya Algeria usiku wa leo atakuwa amefikisha mabao 16 na kumpiku Ronaldo.
Sports4lifetz imebaaini kuwa Ronaldo aliweka rekodi ya kufunga mabao hayo 15 wakati Brazil ikicheza na Ghana katika fainali za kombe la dunia mwaka 2006 pia Klose amefunga bao lake la 15 mchezo dhidi ya Waafrika yaani Ghana.
Ni wazi kuwa Ronaldo na Klose wameweka rekodi zao mbele ya timu za Afrika ambayo ni Ghana.
Je leo Klose ataweka rekodi mbele ya Algeria ambayo inatoka bara la Afrika?????? swali litapata jibu leo usiku.
Kwa upande wake Thomas Muller akifanikiwa kufunga bao leo atakuwa amefikisha mabao kumi toka aanze kucheza kombe la dunia na litakuwa bao lake la 5 kwa mwaka huu na ataingia kwenye kumi bora.
WACHEZAJI WALIOFUNGA MABAO MENGI KOMBE LA DUNIA
   Mchezaji/Nchi     Mabao   
Ronaldo-Brazil 15
Miroslav Klose-Ujerumani 15
Gerd Muller-Ujerumani 14 
 Just Fontaine-Ufaransa 13
 Pele-Brazil 12 
 Sandor Kocsis-Hungary 11 
 Jurgen Klinsmann-Ujerumani 11 
 Helmut Rahn-Ujerumani 10 
 Gary Lineker-uingereza 10 
 Gabriel Batistuta-Argentina 10 


0 comments:

Post a Comment