Wednesday, 25 June 2014

Kombe la dunia Uruguay,Ugiriki mambo safi Ivorycoast kurudi nyumbani


Ugiriki wamefuzu kuingia Raundi ya Pili ya Mtoano ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil baada mkwaju wa pelnati Dakika ya 90 kuwapa ushindi wa mabao 2-1 walipocheza na Ivory Coast kwenye Mechi ya mwisho ya Kundi C.

Mabao yalifungwa na Georgios Samaras anaechezea Celtic ya Scotland na la kwanza lilifungwa na Samaris Dakika ya 42 lakini Ivory Coast walisawazisha kwa Bao la Wilfried Bony na Sare ingeweza kuwafanya wafuze.
Lakini Dakika za Majeruhi, Refa Carlos Vera wa Ecuador alitoa Penati kwenye Dakika za Majeruhi kwa Rafu aliyofanyiwa Samaras na Giovanni Sio  na kuonekana utata.
Penati hiyo ilifungwa Dakika ya 93 na Samaras.
Mapema jana Uingereza wameiaga Brazil rasmi baada ya kutoshinda hata Mechi moja ya Fainali za Kombe la Dunia kwa kumaliza Mechi zao za Kundi D kwa kutoka suluhu Costa Rica ambao kabla ya Mechi hii walikuwa tayari wameshatinga Raundi ya Pili ya Mtoano.
Kocha Roy Hodgson jana aliipangua Timu yake na kuwapa nafasi Wachezaji wengi ambao hawakucheza Mechi mbili za kwanza walizofungwa na Italia 2-1 na Uruguay 2-1.
Italy wametupwa nje ya Kombe la Dunia na Uruguay baada ya kufungwa Bao 1-0 huku wakicheza wachezaji 10 kufuatia Kadi Nyekundu kwa Claudio Marchisio kwenye Dakika ya 60.
Mbali ya kufungwa na kupewa Kadi Nyekundu, hasira kubwa za Italy zipo kwa Refa Marco Rodriguez wa Mexico kwa kutoona Luis Suarez akimng’ata Meno Beki wa Italy Chiellini.
Bao la ushindi la Uruguay lilifungwa kwa Kichwa na Beki Diego Godin katika Dakika ya 81.
Toka Kundi D, Costa Rica na Uruguay zimesonga Raundi ya Pili ya Mtoano na Italy na England kutupwa nje.

0 comments:

Post a Comment