Manchester United yakaribia kumnasa Herrera.
Manchester United wanakaribia kumsaini Kiungo wa Athletic Bilbao, Ander Herrera, kwa Dau la Pauni Milioni 30.
Msimu uliopita, katika Siku ya mwisho ya Dirisha la Uhamisho, Man United walishindwa kumsaini Kiungo huyo mwenye Miaka 24.
Dili hii inatarajiwa kukamilika baadae
hii Leo na Herrera atakuwa Mchezaji wa kwanza kununuliwa na kocha mpya
wa Man United, Louis van Gaal, ambae hivi sasa yuko Brazil akiiongoza
Timu ya Taifa ya Uholanzi ambayo itacheza na Mexico kwenye hatua ya mtoano Fainali za Kombe la Dunia.
Kununuliwa kwa Herrera, ambaye ndiye
alikuwa Kiungo nguzo ya Atletico Madrid iliyotwaa Ubingwa wa La Liga
huko Hispania, kutaimarisha idara ya Kiungo ya Man United iliyodhoofika kwa
kustaafu Paul Scholes na, ukimwondoa Marouane Fellaini aliyesainiwa
Msimu uliopita, haijanunua Kiungo yeyote kwa Miaka 6 sasa.
Ingawa yuko huko Brazil, Van Gaal, ambae
ataanza kazi yake rasmi Old Trafford baada kumalizika kwa Fainali za
Kombe la Dunia, ameshaanza kujenga Kikosi kwa kuwaongezea Mikataba
Antonio Valencia ns Patrice Evra.
0 comments:
Post a Comment