KOZI YA UKOCHA LESENI B YAFIKIA TAMATI
Kozi ya makocha wa mpira wa miguu ya
Leseni B inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF)
iliyodumu kwa wiki mbili inafungwa kesho (Juni 20 mwaka huu) jijini Dar
es Salaam.
Makocha 26 kutoka Tanzania Bara na
Zanzibar wameshiriki katika kozi hiyo chini ya wakufunzi wa CAF, Sunday
Kayuni, Salum Madadi wa Tanzania na Honory Janza kutoka Zambia. Ufungaji
wa kozi hiyo unatarajiwa kufanywa saa 5 asubuhi kwenye hosteli za TFF
zilizopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.
Walioshiriki kozi hiyo ni Abdalla
Mohammed Juma (Zanzibar), Abdul Banyai (Temeke), Abdul Nyumba (Temeke),
Abdulmutik Haji (Zanzibar), Aley Mohammed (Zanzibar), Ali Vuai Shein
(Zanzibar), Dennis Kitambi (Morogoro), Dismas Haonga (Ilala), Emmanuel
Massawe (Shinyanga), Fikiri Elias (Arusha), Fulgence Novatus (Mwanza),
Hababuu Ali Omar (Zanzibar), Juma Mgunda (Tanga) na Kidao Wilfred
(Ilala).
Wengine ni Maka Mwalwisi (Mbeya), Malale
Hamsini Keya (Zanzibar), Mecky Maxime (Morogoro), Mohammed Tajdin
(Temeke), Mussa Furutuni (Dodoma), Nassor Salum Mohamed (Zanzibar),
Peter Mhina (Ruvuma), Said Mohamed Abdulla (Zanzibar), Salim Makame
(Zanzibar), Salum Ali Haji (Zanzibar), Sebastian Nkoma (Ilala), Wane
Mkisi (Dar es Salaam).
0 comments:
Post a Comment