Matokeo ya jana na Ratiba ya leo kombe la dunia.
Mechi za Pili kwa Kundi A la Fainali za Kombe la Dunia zimeanza Estadio Castelão, Fortaleza na Wenyeji Brazil kutoka suluhu kwa maana ya 0-0.
Suluhu hii imeibakisha Brazil juu kwenye Kundi wakiwa na alma 4 sawa na Mexico.
Wakati Kipindi cha Kwanza kilikuwa vuta
ni kuvute ingawa Neymar alikosa Bao la Kichwa ambacho Kipa Ochoa aliokoa
vizuri, Kipindi cha Pili Brazil,walikuja juu na
kukosa mabao kadhaa huku Kipa Ochoa akiokoa mabao mengi na aliinusuru Mexico.
Wakati Mechi ya Kundi F iliyochezwa Arena Pantanal, Cuiba kati ya Urusi na Korea
Kusini ilimalizika kwa sare ya 1-1.
Korea walitangu;ia kufunga katika
Dakika ya 68 kwa Bao la Lee Keun-ho na Mapema Jana, kwenye Mechi ya
kwanza ya Kundi F, Ubelgiji iliifunga Algeria 2-1.
Jumatano ni zamu ya Cameroon na Croatia kucheza Mechi zao za Pili za Kundi A baada ya wote kupoteza Mechi zao za kwanza.
Mechi ya mwisho Brazil watacheza na Cameroon huko Nacional, Brasilia Jumatatu Juni 23 na wakati huo huo Mexico kuivaa Croatia.
Ratiba ya leo
JUMATANO, JUNI 18, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Australia v Netherlands |
B |
Estadio Beira-Rio |
2200 |
Spain v Chile |
B |
Estadio do Maracanã |
0100 |
Cameroon v Croatia |
A |
Arena Amazonia |
0 comments:
Post a Comment