Tuesday, 17 June 2014

Mieleka wanaume watakaopigana kwenye Money in the bank Hawa hapa.

Hatimaye idadi ya watakaoshindania WWE Money in the Bank imekamilika ambapo wanamieleka Roman Reigns, John Cena, Randy Orton, Bray Wyatt, Bingwa wa Marekani  Sheamus, Cesaro na  Alberto Del Rio watashindana katika mchezo unaohusisha ngazi ili kumpata bingwa mpya wa uzito wa juu duniani.
Hapo kabla bingwa anayemiliki mkanda huo Daniel Bryan amejitoa rasmia  June 9 baada ya  kutopona vema na bado hajakamilisha matibabu yake,mchezo huo ni June 29.
Kwenye historia  Cena, Del Rio, Sheamus na Orton wamewahi kuchukua ubingwa huo wa dunia lakiini  Reigns, Wyatt na  Cesaro hawajawahi kubeba ubingwa huo.
Money in the bank ni mchezo ambao wanamieleka hupigana na kisanduku  kufungwa  juu na kuning'inia na atakayeshinda ataweka ngazi ili atoe mkanda huo na ndipo atakuwa mshindi .
Kwa matokeo na nini kinaendelea usikose kufuatilia mtandao huu Sports4lifetz

 

0 comments:

Post a Comment