Sunday, 1 June 2014

Pigo kwa Italia Montolivo kukosa kombe la dunia,avunjika.............


Timu ya taifa ya Italia imepata pigo  kuelekea kombe la dunia baada ya kiungo wake  Riccardo Montolivo kuvunja sehemu ya chini ya goti lake wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya  Ireland katika dimba la  Craven jumamosi hii.
"Ni kitu ambacho tulihofia, kuvunjika. inaweza ikamgharimu zaidi ya mwezi mzima, Riccardo atakuwa nje ya kombe la dunia. Hastahili kuwepo," dakatari wa timu  Enrico Castellacci aliliambia kituo cha Tv cha Rai.
Mchezaji huyo wa  AC Milan  alipata ajali baada ya kukutana uso kwa uso na mlinzi  Alex Pearce katika dakika ya 10 na ilimlazimu kutibiwa zaidi ya dakika 5 uwanjani kabla ya kutolewa kwa machela.
Alipelekwa hospitalini na vipimo vya  X-ray kuonesha kuwa amevunjika.
Nafasi ya  Montolivo ilichukuliwa na  Alberto Aquilani, aliyecheza kwa dakika 23 kabla ya kutolewa baada ya kuumizwa pia na timu hizo kutoka 0-0.
 Kocha Cesare Prandelii  amehuzunishwa na matukio yaliyotokea katika mchezo huo

0 comments:

Post a Comment