Gerard astaafu soka la kimataifa,Soma wasifu wake.
Kiungo wa klabu ya Liverpool na nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza Steven Gerrard amestaafu kucheza soka la kimataifa.Gerrard, mwenye miaka 34 aliiongoza Uingereza katika fainali za kombe la dunia mwaka huu kule Brazil ambapo Uingereza iliondolewa katika hatua ya makundi.
Kiungo huyo kwa mara ya kwanza alianza kucheza soka mwaka 2000 mchezo dhidi ya Ukraine backmwezi mei na kuichezea Uingereza michezo 114 na kufunga mabao 21.
Akizungumza kwenye tovuti ya chama cha soka cha Uingereza FA amesema: "nimefurahia kila dakika niliyowakilisha nchi yangu na ni siku ya masikitiko kufahamu sitovaa tena jezi ya Uingereza.".
Gerard amesemabaada ya kurudi kutoka Brazil amefanya majadiliano na marafiki zake pamoja na familia yake.
Gerard amesema ameelekeza nguvu zake katika klabu ya Liverpool na atajituma zaidi katika michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya msimu huu.
Wasifu | |||
---|---|---|---|
Jina kamili | Steven George Gerrard | ||
Kuzaliwa | 30 May 1980 | ||
Mahali alipozaliwa | Whiston, Merseyside, England | ||
Nafasi Uwanjani | Kiungo | ||
Klabu | |||
Kwa sasa
|
Liverpool | ||
Jezi namba | 8 | ||
Timu ya vijana | |||
1987–1998 | Liverpool | ||
wakubwa | |||
Mwaka | timu | michezo | Mabao |
1998– | Liverpool | 475 | (111) |
Timu ya taifa | |||
1999–2000 | England U21 | 4 | (1) |
2000–2014 | England | 114 | (21) |
0 comments:
Post a Comment