Manchester United na Adidas zakubaliana mkataba mnono,mkataba ni balaa dunia nzima.
Klabu ya Manchester United Leo hii imetangaza kufikia
makubaliano na Kampuni ya Adidas ya Miaka 10 ya Jezi na Vifaa vya
Michezo ambapo watalipwa €940 million na hii ndiyo Dili kubwa
Duniani kwa Mikataba ya aina hiyo.
Kwa mujibu wa mtandao wa Goal.com Mkataba
wa pande hizo mbili utaanza Msimu wa Mwaka 2015/16 na kila Mwaka Man
United italipwa Pauni Milioni 94 ikiipita Real Madrid ambayo ilikuwa
ikizoa Pauni Milioni 31 kwa Mwaka pia kutoka kwa Adidas.
Taarifa hiyo imeendelea kudai zaidi kuwa Msimu huu unaokuja, wa 2014/15, Man United itamaliza Mkataba wa kuvaa Jezi za Nike ambazo wamekuwa nazo kwa Miaka 13 hadi sasa.
Mkurugenzi mtendaji wa Adidas Herbert Hainer amesema kuwa wamevutiwa na klabu hiyo,amabpo amedai kuwa ni timu bora na inayopendwa na watu wengi duniani.
DILI KUBWA ZA JEZI:
TIMU
|
KAMPUNI
|
KWA MWAKA
|
MIAKA
|
JUMLA
|
Manchester United
|
Adidas
|
£94m
|
10
|
£940m
|
Real Madrid
|
Adidas
|
£31m
|
8
|
£248m
|
Chelsea
|
Adidas
|
£30m
|
10
|
£300m
|
Arsenal
|
Puma
|
£30m
|
5
|
£170m
|
Barcelona
|
Nike
|
£27m
|
10
|
£270m
|
Liverpool
|
Warrior
|
£25m
|
6
|
£150m
|
Manchester City
|
Nike
|
£12m
|
6
|
£72m
|
0 comments:
Post a Comment