Thursday, 17 July 2014

Mkongwe EL Hadary kurudi Zamalek lakini Mido amgomea.

Klabu ya  Zamalek ya Misri imefikia makubaliano na golkipa mkongwe  Essam El Hadary ili arudi tena kuitumikia klabu hiyo kwa msimu unaofuata..
Kipa huyo mwenye miaka 41 bado ana mkataba wa miaka miwili  na klabu ya Wadi Degla.
Taarifa za ndani kutoka huko Misri ambazo zimenaswa na Sports4lifetz zimeeleza kuwa  El Hadary alikutana na mwenyekiti Mortada Mansour na kufikia makubalianao ambapo kipa amesema kuwa atavunja mkataba na klabu yake ya   Degla.
Kipa wa sasa wa klabu ya Zamalek Abdel Wahed Al Sayed mapema mwaka huu alitangaza kuwa ligi ikimalizika atatangaza kustaafu soka.
Zamalek imejaribu kuongea na makipa wengi wa pale Misri lakini wamegoma kujiunga mfano kipa wa  Al Ismaily  Mohamed Awad na kipa wa  Al Masry Ahmed El Shenaway.
El Hadary alianza kucheza akiwa na klabu ya  Damietta akajiunga na  Al Ahly mwaka  1996 hadi 2008 akajiunga na FC Sion hadi 2009  kabla ya kujiunga na  Al Ismaily 2009 hadi 2010 halafu akajiunga na Zamalek mwaka 2010  lakini akatimkia klabu  Al-Merreikh ya Sudan na  2013 akajiunga na Wadi Degla.
Lakini kocha wa  Zamalek Ahmed Hossam Mido amemwambia mwenyekiti wake kuwa hataki kumwona Al Hadary katika klabu

0 comments:

Post a Comment