Neymar nje kombe la dunia
Mchezaji nyota wa Brazil Neymar hatachezea nchi yake mashindano ya kombe la dunia yanayoendelea kule Brazil kwa mwaka 2014 baada ya kuumia sehemu inayoshikana na mgongo yaani vertebra na aliumia jana Brazil ikicheza dhidi ya Colombia,ameeleza dakatari wa timu ya Brazil.![]() |
Neymar anaangushwa na Zuniga dk ya 88 |
Dakatari wa timu Rodrigo Lasmar amesema Neymar amevunjika mfupa wa tatu katika mgongo yaani vertebra.
![]() |
Marcelo akilalama kwa mwamuzi baada ya Neymar kuangushwa chini. |
"Jeraha hilo halihitaji upasuaji ila kuna matibabu yake maalum"alisema Lasmar
![]() | |
Neymar akisikilizia maumivu |
Nahodha Thiago Silva alifunga bao la kwanza akipokea mpira kutoka kwa Neymara ambaye aliumia na alishindwa kufurukuta mbele ya Mabeki wa Colombia.
Dakika ya 69 beki David Luiz ambaye kwa sasa amehamia PSG akafunga bao la pili na la ushindi baada ya mpira wa adhabu mita 30 kutoka langoni.
Thiago Silva atakosa mchezo wa nusu fainali baada ya kupewa kadi ya njano,Brazil itapambana na Ujerumani ambayo imeshinda 1-0 dhidi ya Ufaransa.Baada ya mchezo kumalizika Silva alisema kuwa pengo lake litazibwa katika mchezo unaofuata "Nina furaha kwa sababu nilijitolea kwa moyo wangu kuitumikia timu,sitakuwepo mchezo unaofuata ila Dante na Henrique watacheza vizuri." alisema Silva akihojiwa baada ya mchezo kumalizika.
0 comments:
Post a Comment