Ratiba ya leo(Julai 5) mpaka fainali
Baada ya Ijumaa (Julai 4) kushuhudiwa Brazil na Ujerumani wakitinga hatua ya nusu fainali,leo kama kawaida ratiba ya michezo hii yenye raha ya aina yake itaendelea kwa timu nyingine kutafuta hatua ya nusu fainali.Hapo kabla Timu zilizoingia robo fainali ni Wenyaji Brazil, ambao ni Mabingwa wa Dunia mara 5, wapo Mabingwa wengine wa zamani Ufaransa,Ujerumani na Argentina lakini pia zipo timu ambazo hazijawahi kutwaa Kombe hili ambazo ni Colombia, Ubelgiji,Uholanzi na Costa Rica.
Brazil iliingia robo fainali baada ya kuitoa Chile kwa mikwaju ya pelnati vilevile Ujerumani iliitoa Algeria katika muda wa nyongeza wakati Ubelgiji nao iliwachukua mpaka muda wa nyongeza kuwatoa Marekani.
Aidha Costa Rica mikwaju ya pelnati iliwapeleka hatua hii baada ya kuwafunga Ugiriki.
Uholanzi na Ufaransa waliingia baada ya kushinda katika dakika 90 za mchezo,Uholanzi ikiwatoa Mexico wakati Ufaransa iliwachomoa mabingwa wa Afrika Nigeria.
JUMAMOSI, JULAI 5, 2014 | |||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
1900 | Argentina v Ubelgiji [59] | ROBO FAINALI | Nacional, Brasilia | ||||||
2300 | Uholanzi v Costa Rica [60] | ROBO FAINALI | Arena Fonte Nova, Savador | ||||||
NUSU FAINALI JUMANNE, JULAI 8, 2014 |
|||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2300 | Ujerumani v Brazil [61] | NUSU FAINALI | Estadio Mineirão, Belo Horizonte | ||||||
JUMATANO, JULAI 9, 2014 | |||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2300 | Mshindi kati ya Argentina v Ubelgiji v Mshindi kati ya Uholanzi v Costa Rica [62] | NUSU FAINALI | Arena Corinthians, Sao Paulo | ||||||
MSHINDI WA TATU JUMAMOSI, JULAI 12, 2014 |
|||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2300 | Aliyefungwa 61 v Aliyefungwa 62 | MSHINDI WA 3 | Nacional, Brasilia | ||||||
FAINALI JUMAPILI, JULAI 13, 2014 |
|||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2200 | Mshindi Mechi 61 v Mshindi Mechi 62 | FAINALI | Estadio do Maracanã, Rio de Janeiro |
0 comments:
Post a Comment