Saturday, 5 July 2014

Mabeki wa PSG waipeleka Brazil nusu fainali,Rodriguez apiga la 6

Timu ya taifa ya Brazil imefuzu hatua ya nusu fainali za kombe la dunia mashindano yanayofanyika kule kwao baada ya kuibugiza timu ngumu ya Colombia mabao 2-1.
Mabeki mahiri wa klabu ya PSG Inayoshiriki ligi kuu ya Ufaransa Thiago Silva na David Luiz walikuwa shujaa katika mchezo uliomalizika muda mfupi uliopita katika dimba la Castela mjini Forteleza.
Nahodha  Thiago Silva  alifunga bao la kwanza  akipokea mpira kutoka kwa Neymara ambaye leo alishindwa kufurukuta mbele ya Mabeki wa Colombia.
Dakika ya  69 beki David Luiz ambaye kwa sasa amehamia PSG akafunga bao la pili na la ushindi baada ya mpira wa adhabu  mita 30 kutoka langoni,
Mfungaji wa bao la pili,David Luis
Colombia ilipata bao lakini likakataliwa na mwamuzi  Carlos Vellasco kutoka Hispania kabla ya mchezaji ambaye yuko kwenye kiwango cha juu James Rodriguez hajafunga bao lake la 6 la mashindano ya mwaka huu na kuwa mfungaji anayeongoza mpaka sasa,alifunga kwa njia ya pelnati na kuwa 2-1.
Thiago Silva atakosa mchezo wa nusu fainali baada ya kupewa kadi ya njano,Brazil itapambana na Ujerumani ambayo imeshinda 1-0 dhidi ya Ufaransa.
ALIFUNGA LA KWANZA,THIAGO SILVA
Baada ya mchezo kumalizika Silva alisema kuwa pengo lake litazibwa katika mchezo unaofuata "Nina furaha kwa sababu nilijitolea kwa moyo wangu kuitumikia timu,sitakuwepo mchezo unaofuata ila Dante na Henrique watacheza vizuri." alisema Silva akihojiwa baada ya mchezo kumalizika.
Lakini Neymar aliumia na kukimbizwa hospitalini baada ya kukumbana na Juan Camillo Zuniga akilalamika maumivu ya mgongo.

0 comments:

Post a Comment