Suarez ndani ya saa 24 atakuwa mali ya Barcelona,daktari kwenda kumpima akiwa Uruguay
Maelewano hayo yamedumu kwa takribani wiki nzima baina ya vilabu viwili na atatangazwa ndani ya saa 24 kuwa mali halali ya Barcelona.
Barcelona wanafanikiwa kumdaka Suarez na wanatakiwa kutoa hela moja kwa moja baada ya Suarez kusaini mkataba mwezi disemba na Liverpool.
Inasadikiwa kuwa Suarez atapimwa vipimo vya afya akiwa nchini kwao Uruguay, baada ya kupewa adhabu na FIFA kwa kisa cha kumng'ata meno beki wa Italia Chiellini katika kombe la dunia,na Barca tayari imekwishamtuma daktari wake.
Kila kitu kinakwenda vema ila kilichobaki ni Suarez kutangazwa ili awe mchezaji halali wa Barcelona,imeeleza taarifa ya mtandao wa Goal.com
Barca imeamua fedha za kumuuza Alexis Sanchez kwenda Arsenal itatumika kama sehemu ya dili hilo.
Liverpool kwa sasa wanajiimarisha zaidi na wamekaribia kabisa kuwanasa wachezaji watatu ambao ni winga wa Benfica Lazar Markovic, mshambuliaji wa Lille Divock Origi na mlinzi wa Southampton Dejan Lovren.
0 comments:
Post a Comment