Sunday, 20 July 2014

Tetesi za usajili jumapili.(Julai 20)

Klabu ya Manchester United itatoa kiasi cha  £10 million kwa ajili ya mlinzi wa  Arsenal Thomas Vermaelen.
Klabu ya  Paris Saint-Germain inakaribia kumnasa mchezaji  Angel Di Maria,mchezaji huyo amekubali kujiunga wakati huo  Edinson Cavani anataraji kwenda Manchester United

Klabu ya Manchester United wamerudisha tena nia yao ya kumsajili mchezaji wa  Paris Saint-Germain Edinson Cavani iwapo Wayne Rooney atashindwa kumshawishi vizuri  Louis van Gaal.

Kocha wa Manchester United  Louis van Gaal ameandaa kiasi cha  €12.5 million kwa ajili ya kumnasa mlinzi wa kati wa  Feyenoord  Stefan de Vrij.

Liverpool wao wameanza kumsaka mchezaji wa Man city James Milner
Everton ina imani kuwa  Romelu Lukaku atajiunga nao ila  Chelsea wanataka kiasi cha  £20 million kwa ajili ya nyota huyo wa Ubelgiji.
Liverpool iko mbioni kumsajili kipa wa Fiorentina  Neto baada ya kipa wa Swansea City Michel Vorm ugoma kujiunga nao.

0 comments:

Post a Comment