Waliowahi kutwaa tuzo ya Golden Ball tokea 1930 hwa hapa
Fainali za kombe la dunia Zitahitimishwa leo kwa mchezo wa fainali kati ya Ujerumani na Argentina na Shirikisho la soka duniani FIFA imetangaza Majina ya Wachezaji 10 watakaogombea Tuzo ya Mchezaji Bora wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil, Tuzo ya Mpira wa Dhahabu.Listi hiyo ya Wachezaji 10 inao Wachezaji Wanne kutoka Ujerumani, Watatu wa Argentina huku Colombia, Brazil na Uholanzi zikitoa Mchezaji mmpja moja.
Wachezaji wa Argentina ambao wako kwenye Lisi hiyo ni Angel Di Maria, Javier Mascherano na Lionel Messi.
Ujerumani ni Mats Hummels, Toni Kroos, Phillip Lahm na Thomas Muller.
Waliobaki ni Straika wa Colombia James Rodriguez, Nyota wa Brazil Neymar na Arjen Robben wa Uholanzi.
‘GLOVU YA DHAHABU’
Vile vile FIFA imateja Majina ya Makipa Watatu ambao watawania Tuzo ya Kipa Bora wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil.
![]() |
Manuel Neur |
Makipa hao ni Kipa wa Costa Rica Keylor Navas, Manuel Neuer wa Germany na Kipa wa Argentina Sergio Romero.
‘MCHEZAJI BORA KIJANA’
Pia, mshambuliaji wa Uholanzi Memphis Depay pamoja na Paul Pogba na Raphael Varane wa Ufaransa wameteuliwa kugombea Tuzo ya Mchezaji Bora Kijana.
Washindi wote wa Tuzo hizo watatangazwa mara baada ya Fainali ya Jumapili kati ya Argentina na Ujerumani huko Estadio Maracana, Rio de Janeiro.
Waliowahi kutwaa tuzo hizo |
|
---|---|
1930 | Jose Nasazzi (Uruguay) |
1934 | Giuseppe Meazza (Italy) |
1938 | Leonidas (Brazil) |
1950 | Zizinho (Brazil) |
1954 | Ferenc Puskas (Hungary) |
1958 | Didi (Brazil) |
1962 | Garrincha (Brazil) |
1966 | Bobby Charlton (England) |
1970 | Pele (Brazil) |
1974 | Johan Cruyff (Netherlands) |
1978 | Mario Kempes (Argentina) |
1982 | Paolo Rossi (Italy) |
1986 | Diego Maradona (Argentina) |
1990 | Salvatore Schillaci (Italy) |
1994 | Romario (Brazil) |
1998 | Ronaldo (Brazil) |
2002 | Oliver Kahn (Germany) |
2006 | Zinedine Zidane (France) |
2010 | Diego Forlan (Uruguay) |
0 comments:
Post a Comment