Washauri wa FIFA na pendekezo la wachezaji wanne wa akiba.
Jopo la Washauri wa Masuala ya Makocha
la Shirikisho la soka Ulimwenguni FIFA linatafakari kutoa mapendekezo kwa FIFA kuruhusu idadi ya
Wachezaji wa Akiba wanaotoka Benchi na kuruhusiwa kucheza iwe Wanne
badala ya Watatu wa sasa.
Lakini Jopo hilo linataka Mchezaji huyo
wa Nne atakaeruhusiwa awe anaingizwa wakati wa Nyongeza za Dakika 30
baada ya Timu kwenda Sare katika Dakika 90.
Mmoja wa Wajumbe wa Jopo hilo Kocha wa zamani wa Liverpool, Gerard
Houllier amesema: “Ni wazo zuri
ambalo tutalipeleka kwenye Vikao vya Kutunga Sheria FIFA!”
Houllier, ambae pia aliwahi kuwa Kocha
wa Ufaransa, amefafanua kuwa kuruhusu Mchezaji wa 4 kuingia kwenye Dakika
za Nyongeza 30 itasaidia kupunguza athari za Wachezaji kubanwa na Msuli
wakati huo na kuzipa nafuu Timu.
Aidha Houllier amesisitiza Wachezaji
wanaotoka Benchi wana mchango mkubwa wa kubadilisha matokeo ya Mechi
kwani huko Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia Wachezaji waliotoka
Benchi na kuingizwa wamefunga mabao 29 na kuvunja Rekodi ya Fainali za
Kombe la Dunia za Mwaka 2006 huko Ujerumani walipofunga mabao 23 na bado Mechi 8 hazijachezwa.
Houllier amesema: “Wachezaji wa Akiba
wana umuhimu mkubwa kwa sababu wanaingia wakiwa na akili mpya. Karibu
robo ya Magoli yamefungwa kwenye Robo Saa ya mwisho huko Brazil. ”
Baadhi ya Magoli hayo ni mchango wa
Klaas-Jan Huntelaar alipoingizwa Dakika ya 76 kutoka Benchi na kuisaidia Uholanzi kwa kumpasia Wesley Sneijder Dakika ya 88 na kusawazisha na
kisha yeye mwenyewe kufunga Bao la Pili na la ushindi kwa Penati ya
Dakika ya 94 walipoibwaga Mexico 2-1.
Naye Kipa wa Marekani
Tim Howard kuizuia Ubelgiji na kutoka suluhu katika Dakika 90,
akaingizwa Romelu Lukaku ambaye, katika Dakika za Nyongeza 30, alimpasia
Kevin De Bruyne aliyefunga Bao la kwanza na yeye mwenyewe kupiga Bao la
pili na Ubelgiji kushinda 2-1.
Mwaka 2012, FIFA iliwahi kuyakataa
mapendekezo ya aina hii hii ya kuongeza Wachezaji wa Akiba kuruhusiwa
kucheza kuwa Wanne lakini safari hii Houllier anaamini yatapitishwa.
0 comments:
Post a Comment