Majina ya Waamuzi wa robo fainali kombe la dunia
Shirikisho la soka duniani FIFA limetangaza Majina ya waamuzi watakaochezesha Mechi za Robo Fainali za Kombe la Dunia,Brazil 2014.
Waamuzi waliotangazwa ni michezo ya Ufaransa v Ujerumani, Brazil v Colombia
Michezo hiyo itapigwa kesho julai 4, 2014
![]() |
| Nestor Pitana |
Mechi ya kwanza
ya Ijumaa kati ya Ufaransa na Ujerumani,Nestor Pitana atasimamia na hii itakuwa ni Mechi ya 4 kwa mwamuzi huyo kutoka Argentina kuchezesha huko Brazil.
Pitana, mwenye Miaka 39, alichezesha
Mechi za Makundi huko Brazil kati ya Urusi na Korea , Marekani na Ureno na Honduras dhidi ya Switzerland.
Mechi ya Wenyeji Brazil na Colombia itachezeshwa na mwamuzi wa Hispania Carlos Velasco.
![]() |
| Carlos Velasco |
Velasco, mwenye Miaka 43, amebahatika kusimamia
Mechi 2 huko Brazil ambazo ni zile za Makundi kati ya Uruguay na Uingereza
na ile ya Bosnia and Herzegovina dhidi ya Iran.


0 comments:
Post a Comment