Tuesday, 8 July 2014

Watu mbalimbali kwenye picha wakiwa katika maombolezo ya kifo cha Di Stefano.



Waombelezaji leo wameendelea kutoa heshima zao kwa aliyekuwa gwiji wa klabu ya Real Madrid  Alfredo Di Stefano Wakati jeneza lake liliwekwa katika uwanja wa  Bernabeu.
Di Stefano alifariki jana akiwa hospitalini akiwa na umri wa miaka   88,baada ya kupata mshtuko wa moyo.

Real Madrid legend Alfredo di Stefano
Alfredo Di Stefano:
Di Steafano  alikuwa katika hali ambayo ilikuwa hairidhishi baada ya kupata mshtuko wa moyo katika mji ulio karibu na Santiago Bernabeu siku ya jumamosi, siku chache tu baada ya kuadhimisha sherehe ya siku yake ya kuzaliwa kutimiza miaka  88,amefariki baada hali yake kuwa mbaya asubuhi ya jana.
Di Stefano alianza kucheza soka akiwa na klabu ya River Plate baadaye akajiunga na  Madrid akitokea klabu iliyopo nchini Colombia, Millonarios Mwaka  1953, kabla ya hapo alikaribia kujiunga na Barcelona.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa  Argentine aliitumikia Madrid kushinda mataji 8 ya  Liga na mataji 5 ya ligi ya mabingwa kati ya 1953 na 1964.

Amefunga mabao  308 katika michezo 396 kwa upande wa Real na nabaki kuwa mfungaji bora wa pili wa Madrid nyuma ya  Raul (323). Mchezaji bor wa dunia  Cristiano Ronaldo ameandika katika twita yake kuwa gwiji hafi daima,tunakushukuru.
Florentino Perez stands next to the coffin of the late Alfredo Di Stefano
Rais Florentino Perez wa Real Madrid akisimama karibu na jeneza ambalo lina mwili wa marehemu  Alfredo Di Stefano
The wake for former Real Madrid great Alfredo Di Stefano
Watu wakitoa heshima zao
Family members and friends pay their respects to Alfredo Di Stefano at the Santiago Bernabeu
FFamilia na marafiki wakitoa heshima zao hii leo
A man writes a message on a wall to pay tribute to Real Madrid's late honorary president Alfredo Di Stefano
Mshabiki huyu akiandika ujumbe kama kumbukumbu kwa ajili ya gwiji wao .
Real Madrid goalkeeper Iker Casillas greets other mourners by the coffin of Alfredo Di Stefano
Kipa wa Real Madrid  Iker Casillas alikuwepo kwenye maombolezo ya marehemu Di Stefano

0 comments:

Post a Comment