Maximo ameamua mwaka huu,kuongea na wanahabari kila siku Ijumaa.
Kocha mkuu wa timu ya Young Africans SC Mbrazil Marcio Maximo
amesema atakua akiongea na waandishi wa habari kila siku ya Ijumaa
asubuhi mara tu baada ya mazoezi katika shule ya sekondari Loyola ili
kuwapa fursa ya kumuuliza maswali mbalimbali kuhusiana na
maandalizi ya kikosi chake msimu ujao, taarifa kwa mujibu wa mtandao wa Yanga.
Maximo amesema, ameamua kufanya hivyo ili kupunguza kuwepo taarifa
tofauti kuhusiana na benchi la ufundi pamoja na wachezaji wake katika
maandalizi ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015.
Unajua
utendaji wa kazi umebadilika, nafasi yangu kwenye klabu na nilipokua
timu ya Taifa ni tofauti, hivyo nimekubaliana na uongozi na umeniruhusu
kuwa naongea na vyombo vya habari kwa pamoja kila siku ya Ijumaa mara tu
baada ya mazoezi ya asubuhi "alisema Maximo"
Yanga imewaomba Waandishi
wa habari, Vyombo vya Habari kuhudhuria kila siku ya ijumaa
shule ya sekondari Loyola ili wapate nafasi ya kuongea na kocha Maximo na
kumuuliza maswali, kwani kwa sasa yeye ndiye atakayekua akiongelea timu,
wachezaji pamoja na benchi lake la ufundi.
Maximo
ameanza kazi ya kukinoa kikosi cha Young Africans tangu mwishoni mwa
wiki iliyopita na kuwatuvia wapenzi, washabik na wanachama ambao wamekua
wakijitokeza kwa wingi kushuhudia ufundishaji wa kocha huyo mwenye
mvuto mkubwa kwenye soka la Tanzania.
0 comments:
Post a Comment