Tuesday, 19 August 2014

Guinea na Siera Leone kucheza Morocco kufuzu AFCON 2015.

Shirikisho la soka nchini Guinea (GFF) Imetangaza kuwa mchezo wa kufuzu AFCON  2015 kati yao na Togo utachezwa nchini Morocco.
Mapema wiki hii  Shirikisho la Soka barani Afrika,CAF imeagiza Guinea kuandaa mechi baina yake na Togo katika taifa mbadala kufuatia mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola.
Mchezo huo wa kundi la  E utapigwa mjini Casablanca hapo Sptemba 5.
Caf pia imsema kuwa  mchezo baina ya Sierra Leone na DR Congo upigwe septemba 10 lakini uwanja wa mchezo huo bado haujajulikana.
Lakini Shirikisho la soka nchini Sierra Leone(SLFA)linaamini kuwa mchezo huo utapigwa nchini Ghana.

0 comments:

Post a Comment