Manchester City na Liverpool leo saa nne usiku,msimamo mpaka sasa.
Raundi ya pili ya ligi kuu ya Uingereza inahitimishwa leo ambapo mabingwa watetezi Manchester City, inayofundishwa na Manuel Pellegrini,itawaalika Liverpool, Timu ambayo Msimu uliopita ilimaliza Nafasi ya Pili.Katika michezo zao za awali timu zote zilishinda.
Man City walianza Ugenini huko St James Park na kuifunga Newcastle mabao 2-0 na Liverpool wakiwa Anfield walishinda mabao 2-1 walipoifunga Southampton huku Bao la ushindi likifungwa mwishoni na Daniel Sturridge.
Kuelekea mchezo huo utakaopigwa saa nne kamili usiku Manchester City kuna uwezekano wa Edin Dzeko na Stevan Jovetic kuanza Mechi hii kwani Sergio Aguero bado hajawa fiti kucheza Mechi kwa Dakika 90 kufuatia kuwa Majeruhi.
Liverpool huenda wakawatumia wachezaji wao wapya, Kiungo wa Serbia Lazar Markovic na Beki Alberto Moreno
MSIMAMO BAADA YA MECHI ZA JANA
| |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||

0 comments:
Post a Comment