Wednesday, 17 September 2014

Dunga ataja kikosi cha kuivaa Argentina,Maicon na Marcelo nje.

Kocha wa Brazil Dunga ametaja kikosi cha wachezaji  22 kwa ajili ya mechi za kirafiki dhidi ya  Argentina na Japan mwezi ujao.

Mabingwa hao mara tano wa kombe la dunia watakwenda mjini  Beijing hapo Octoba 11 kupambana na makamu bingwa wa kombe la dunia na kuelekea  Singapore kupepetana na Japan Octoba 14.

Kuna wachezaji wawili tu walioitwa kwenye kikosi hiki tofauti na ile ya awali ambapo  mchezaji wa Inter Dodo na mchezaji wa CSKA Mario Fernandes wameitwa kuziba nafasi za Marcelo na Maicon


KIKOSI KAMILI
Makipa: Jefferson (Botafogo), Rafael Cabral (Napoli).

Walinzi: David Luiz (Paris Saint-Germain), Marquinhos (Paris Saint-Germain), Gil (Corinthians), Miranda (Atletico Madrid), Dodo (Internacional), Filipe Luis (Chelsea), Mario Fernandes (CSKA), Danilo (FC Porto).

Viungo: Luiz Gustavo (Wolfsburg), Elias (Corinthians), Fernandinho (Manchester City), Ramires (Chelsea), Willian (Chelsea), Everton Ribeiro (Cruzeiro), Oscar (Chelsea), Coutinho (Liverpool).

Washambuliaji: Ricardo Goulart (Cruzeiro), Robinho (Santos), Neymar (Barcelona), Diego Tardelli (Atletico MG).

0 comments:

Post a Comment