Saturday, 6 September 2014

Kufuzu AFCON Senegal,Afrika Kusini waanza vizuri,pata ratiba ya leo.

Timu ya taifa ya Senegal imeanza vizuri michezo ya  kufuzu AFCON 2015 kutoka kundi   G  baada ya kuwalaza Misri mabao 2-0  kwa mabao ya Mame Diouf na Sadio Mane,mchezio uliopigwa jana

Katika mechi nyingine  kundi A Afrika Kusini wakicheza Mechi yao ya kwanza chini ya Kocha mpya Shakes Mashaba aliyemrithi Gordon Igesund, waliifunga Sudan mabao 3-0 Uwanjani Al Merreikh Mjini Kahrtoum.

Mabao ya Afrika kusini yalifungwa na Sibusiso Vilakazi, mabao 2, na moja la Bongani Ndulula.

Kwenye Mechi nyingine ya Kundi E, Guinea, ikicheza ‘Nyumbani’ Nchini Morocco kutokana na Nchi yao kukumbwa na Ugonjwa wa Ebola, walitoka suluhu Uwanjani Stade Mohammed V Mjini Casablanca.

RATIBA

 Jumamosi Septemba 6  2014
DR CongovCameroon


GuineavTogo


Burkina FasovLesotho


EthiopiavAlgeria


MalivMalawi


Ivory CoastvSierra Leone


GabonvAngola


NigervCape Verde


ZambiavMsumbiji


GhanavUganda


NigeriavCongo


TunisiavBotswana
.

0 comments:

Post a Comment