Tuesday, 30 September 2014

Manchester United na Chelsea kupambana ili kumnasa Coleman,Fellaini itakula kwake.

Klabu ya Manchester United iko kwenye mpango wa kumnunua mlinzi wa  Everton Seamus Coleman wakati huo Marouane Fellaini atahusishwa katika mpango huo.

Gazeti la The Guardian la Uingereza limeeleza kuwa raia huyo wa Jamhuri ya Ireland  ambaye pia anawindwa na Chelsea amevutiwa na kocha Van Gaal.

Van Gaal atapambana na Mourinho katika dili hilo.

Imeelezwa kuwa Kocha wa Chelsea  Jose Mourinho ameridhishwa na kiwango na mchezaji huyo mwenye miaka 25  na atasajiliwa katika usajili wa mwezi Januari.

Manchester United imesema kuwa  itamrudisha kiungo wake ambaye ameshuka kiwango  Marouane Fellaini katika viunga vya Goodison Park.

Fellaini alijiunga na  Manchester United akitokea Everton msimu wa mwaka  2013, wakati huo Red Devils wakifundishwa na David Moyes, lakini (Fellaini) alishindwa kung'aa ndani ya Old Trafford.

0 comments:

Post a Comment