Wednesday, 3 September 2014

Mashindano ya Big Brother yasogezwa mbele,moto wateketeza nyumba.

Uzinduzi wa makala mapya ya kipindi maarufu cha Big Brother nchini Afrika Kusini umeahirishwa baada ya moto mkubwa kuteketeza studio za kipindi hicho mjini Johannesburg.

Kipindi hicho kilistahili kuanza Jumapili Agosti 7  lakini waandaaji wa wa kipindi chenyewe wameamua kuahirisha uzinduzi huku wakitafuta sehemu nyingine ya kupeperushia kipindi hicho.
Hakuna aliyejeruhiwa kwenye mkasa huo wa moto na kilichousababisha bado hakijajulikana kwani uchunguzi unatarajiwa kufanywa.

Washiriki katika kipindi hicho kutoka nchi 14 Afrika watakuwa wanashiriki katika makala ya 9 ya kipindi hicho.
Kipindi chenyewe kinatarajiwa kupeperushwa kwa siku 99 kabla ya mshindi kutangazwa.

0 comments:

Post a Comment