Thursday, 18 September 2014

Ole Gunnar Solskjaer ajiuzulu kuifundisha Cardiff City.

Kocha wa klabu ya Cardiff City Ole Gunnar Solskjaer amejiuzulu kama kocha wa klabu hiyo baada ya kuifundisha kwa miezi minane.

Solskjaer, 41, alitangaza uamuzi huo baada ya kukutana na mwenyekiti wa klabu  Mehmet Dalman.

Klabu hiyo inashika nafasi ya  17 katika timu zinazogombea kupanda EPL na juzi ilipigwa  1-0 na Middlesbrough na kupigwa mabao  4-2 dhidi ya  Norwich.

Mlinzi mkongwe Danny Gabbidon na  Scott Young wataiongoza klabu kwa muda.

Solskjaer alibeba mikoba ya  Malky Mackay  Januari 2014 wakati  Cardiff ikiwa katika ligi kuu.

Mmiliki wa klabu Vincent Tan amesema kuwa walimchukua Ole Gunnar Solskjaer ili  aiokoe timu isishuke daraja lakini kwa bahati mbaya Ole Gunnar Solskjaer alishindwa kuiokoa klabu hiyo.

Rekodi za Ole Gunnar Solskjaer ndani ya Cardiff .

Amecheza mechi: 30
Ameshindas: 9
Sare: 5
Kufungwa: 16

0 comments:

Post a Comment