Thursday, 18 September 2014

VPL kuanza jumamosi Azam na Polisi Moro,Yanga na Mtibwa.











Ligi kuu kandanda Tanzania Bara itaanza kunguruma jumamosi hii Septemba 20 katika viwanja mbalimbali.
Mabingwa watetezi, Azam FC wakifungua dimba na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Yanga SC  wataanza na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro siku hiyo, wakati washindi wa tatu, Mbeya City wataanza na JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Sokoine.

Mechi nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

Mabingwa wa zamani wa ligi hiyo, Simba SC wataanza kampeni ya kutwaa tena taji hilo Septemba 21 dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Raundi ya pili itaendelea Septemba 27 na 28

    SIMBA SC     Vs POLISI MOROGORO    NATIONAL STADIUM
    MTIBWA SUGAR    Vs    NDANDA FC    MANUNGU
    AZAM FC        Vs    RUVU SHOOTINGS    AZAM COMPL
    MBEYA CITY     Vs     COASTAL UNION     SOKOINE     MBEYA    
     MGAMBO JKT     Vs     STAND UNITED     MKWAKWANI     TANGA    
   
     28.09.2014    
       JKT RUVU     Vs KAGERA SUGAR  AZAM COMPLEX     DAR ES SALAAM    
      YOUNG AFRICANS     Vs     TANZANIA PRISONS     NATIONAL STADIUM
                      












































































































0 comments:

Post a Comment