Kuumia kwa Ozil si tatizo kwa Arsenal-Wilshere.
Kiungo wa klabu ya Arsenal Jack Wilshere haamini kuwa kuumia kwa Mesut Ozil ni athari kubwa kwa klabu yao ya Arsenal inayojiandaa kucheza na Hull City katika ligi kuu ya Uingereza.Mjerumani huyo atakaa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi mitatu baada ya kuumia goti na amekuwa mchezaji muhimu katika msimu huu wa 2014-15.
Taarifa zilizonaswa na mtandao huu ni kwamba Wilshere amesema kuwa nafasi ya Ozil itazibwa na Alex Oxlade-Chamberlain na Theo Walcott, ambaye kwa sasa amepona.
"Ozil anacheza upande wa kushoto,atakaa mtu yeyote,"alisema Wilshere.
"Chambo atatumia hiyo nafasi. Theo amepona. Kwa hiyo Theo au Chambo atacheza tu alisema Wilshere.
Ameendelea kusema kuwa kuna wachezaji wengi tu ambao wana uwezo wa kucheza namba 10 kama Ozil.
Ikumbukwe kuwa Ozil atakosa baadhi ya mechi ndani ya Arsenal
ambazo ni
18 October: Hull (H) - Premier League
22 October: Anderlecht (A) - Champions League
25 October: Sunderland (A) - Premier League
1 November: Burnley (H) - Premier League
4 November: Anderlecht (H) - Champions League
9 November: Swansea (A) - Premier League
22 November: Man Utd (H) - Premier League
26 November: Borussia Dortmund (H) - Champions League
29 November: West Brom (A) - Premier
3 December: Southampton (H) - Premier League
6 December: Stoke (A) - Premier League
9 December: Galatasaray (A) - Champions League
13 December: Newcastle (H) - Premier League
21 December: Liverpool (A) - Premier League
26 December: QPR (H) - Premier League
28 December: West Ham (A) - Premier League.

0 comments:
Post a Comment