Messi afikia rekodi ya Raul Ulaya.
Lionel Messi amefungana na nyota wa zamani wa Real Madrid Raul kwa ufungaji wa mabao mengi katika Historia ya ligi ya mabingwa barani ulaya UEFA baada ya Jana kufunga mabao yote 2 wakati Timu yake Barcelona inaichapa Ajax huko Amsterdam, Uholanzi.Rekodi ya Raul ni mabao 71 na mabao hayo ya Messi yamemfanya afikishe mabao 71 huku nyuma yao akiwepo Mchezaji Bora Duniani Cristiano Ronaldo mwenye Mabao 70.
Mabao hayo ya Messi hapo Jana imeifanya Barcelona iungane na Bayern Munich, PSG na FC Porto kufuzu kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCl huku zikiwa zimebakisha Mechi mbili za Makundi.
Wanaoshikilia rekodi ya mabao UEFA.
Lionel Messi mabao 71
Raul mabao 71
Cristiano Ronaldo mabao 70
Ruud van Nistelrooy mabao 56
Thierry Henry mabao 50

0 comments:
Post a Comment