Monday, 17 November 2014

Ulingo wa mieleka John Cena amchapa Randy Orton,Big Show achapwa na Rusev.

Wiki iliyopita wapenda mieleka walishuhudia  wababe mbalimbali wakipanda ulingoni katika mchezo wa Hell in a Cell.

Mwezi mzima ulitawaliwa na maneno ya hapa na pale kutoka kwa wanamieleka huku kila moja akitamba kuwa atamshinda mwenzake.

Mpambano uliokuwa unasubiriwa kwa hamu ni ule kati ya John Cena na Randy Orton ambapo mshindi atacheza na Brock Lesner.

Hatimaye John Cena alitamba kwa mara nyingine baada ya kumpiga mzee wa RKO,Rand Orton na hivyo Cena atapigana na Brock Lesnar ili kugombania ubingwa wa dunia.
 
Matoke mengine.
Seth Rollins alimpiga  Dean Ambrose (Hell in a Cell )
Rusev alimgaragaza  Big Show

Bingwa wa United States  Sheamus alitetea taji lake kwa kumpiga  The Miz


Mabingwa wa dunia katika mchezo wa timu iliyoungana Gold & Stardust walishinda mbele ya The Usos
Bingwa kwa upande wa akina dada maarufu kama Divas Champion AJ Lee alimpiga Paige

Bingwa wa mabara  Dolph Ziggler alishinda mbele ya  Cesaro
Mark Henry alimpiga  Bo Dallas
 



0 comments:

Post a Comment