Wednesday, 19 November 2014

Ureno,Ujerumani na Uingereza washinda mechi za kirafiki.

Usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Old Trafford huko Jijini Manchester ulijaa Washabiki kuwashuhudia Wachezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, wakiongoza Nchi zao kupambana kwenye Mechi ya Kimataifa ya Kirafiki.

Mchezo huo ulimalizika kwa Ureno kushinda 1-0 na ni Bao la Dakika ya 90 la Kichwa cha Raphael Guerreiro ndio liliwapa Ureno ushindi.

Lakini baada ya mchezo kumalizika kocha wa Argentina Tata Martino amesema kuwa timu yake ni bora kuliko Ureno japo wamefungwa.

Katika mchezo huo Ronaldo na Messi walipumzishwa wakati wa mapumziko  na kuonekana kama na msisimko ulipotea baada ya hapo

MATOKEO MENGINE KIMATAIFA KIRAFIKI

Jumanne Novemba 17

Japan 2 Australia 1

Slovakia 2 Finland 1

Belarus 3 Mexico 2

Greece 0 Serbia 2

Slovenia 0 Colombia 1

Austria 1 Brazil 2

Romania 2 Denmark 0

Hungary 1 Russia 2

Italy 1 Albania 0

Poland 2 Switzerland 2

Portugal 1 Argentina 0

Republic of Ireland 4 USA 1

Spain 0 Germany 1

France 1 Sweden 0

Scotland 1 England 3

0 comments:

Post a Comment