Friday, 19 December 2014

Mganda Lure kocha mkuu Stand United ya Shinyanga.



Klabu ya Stand United ya Shinyanga imefanya marekebisho katika Benchi la ufundi baada ya kumchukua  mwalimu Mathias Lure kutoka nchini Uganda  kuwa kocha mkuu.

Lure ambaye mara ya mwisho alikuwa anaifundisha klabu ya Express ya Uganda kama kocha mkuu,na alishawahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana ya nchini humo.


Taarifa ya mtandao wa klabu hiyo imeeleza kuwa klabu imeingia mkataba wa miezi sita na kocha huyo na ameshaanza kazi rasmi huku  akisaidiwa na Emmanuel Massawe kocha msaidizi wa kwanza na Athumani Bilali kocha msaidizi wa pili.


Ikumbukwe kuwa Dirisha dogo la usajili  Tanzania limefungwa na STAND United imesajili wachezaji wafuatao.

Haruna Chanongo kutoka Simba SC(Mkopo),Chinedu Nwankoene (NIGERIA),Hamisi Thabiti Kutoka Yanga (Mkopo),Shaaban Kondo (Tessema fc) inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara,Zuber Ubwa,mtanzania aliyekuwa anacheza soka nchini Ureno katika timu ya daraja la pili.


Wengine ni Hamisi Shengo (mchezaji huru),msimu uliopita alikuwa mchezaji wa Coastal Union ya Tanga Pamoja na  Charles Mishetto aliyekuwa anacheza katika ligi daraja la nne nchini ujerumani.

0 comments:

Post a Comment