Tuesday, 27 January 2015

Leo vita ya Ghana na Afrika kusini,Algeria na Senegal.


Timu za taifa za Ghana na Afrika kusini zinapamba leo usiku katika mechi za mwisho za makundi ya kombe la mataifa barani Afrika nchini Equatorial Guinea.

Kuelekea mchezo huo kocha wa Afrika ya kusini  Shakes Mashaba  amesema leo lazima timu yake ishinde ili kuhakikisha wanaingia hatua ya robo fainali.

Afrika ya kusini Ilifungwa mabao 3-1 na Algeria kabla ya kutoka sare ya 1-1 na Senegal,hivyo wanahitaji kushinda dhidi ya Ghana.

Kocha wa Ghana Avram Grant alipoteza mchezo wa ufunguzi kwa  2-1 dhidi ya  Senegal kabla ya kushinda bao 1-0 dhidi ya Algeria kwa bao la Asamoah Gyan.

Afrika ya kusini itawategemea washambuliajhi  Bongani Ndulula na  Tokelo Rantie  huku mlinzi  Brilliant Khuzwayo  akipewa jukumu la kuwadhibiti washambuliaji wa Ghana.

Ghana itamtegemea zaidi nyota Asamoah Gyan katika nafasi ya ushambuliaji.

Vilevile hii leo Algeria itapambana na Senegal mechio za kundi C.

Iwapo Ghana ikishinda itafikisha alama 6 na kuziba nafasi ya bafanabafana kufuzu lakini bafanabafana nao wakishinda watafikisha alama 4 lakini wana nafasi ngumu ya kusonga mbele.

Ikiwa Algeria na Senegal zitatoka sare  huku Ghana wakifungwa basi zitafuzu hatua ya robo fainal.



0 comments:

Post a Comment