RAUNDI YA PILI TAIFA CUP WANAWAKE JUMAMOSI
Mechi za kwanza za raundi ya pili ya mashindano ya Taifa ya mpira
wa miguu kwa wanawake (Taifa Cup Wanawake) zinachezwa wikiendi hii (Januari 17
mwaka huu) kwenye miji minane tofauti nchini.
Timu tisa zilizofuzu kutoka raundi ya kwanza baada ya mechi za
nyumbani na ugenini akiwemo mshindwa bora (best loser) zitaungana na Ilala, Kinondoni
na Temeke kucheza raundi ya pili. Mechi za marudiano za raundi hiyo zitachezwa
Januari 21 mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment