Thursday, 29 January 2015

Tottenham na Chelsea kupambana fainali ya Capital One.

Klabu ya Tottenham hotspur itapambana na Chelsea katika mchezo wa fainali kombe la Capital One baada ya kufuzu kwa jumla ya mabao 3-2 dhidi ya Shieffield.

Katika mchezo wa kwanza Tottenham ilipata ushindi wa bao 1-0  na jana ilitoka sare ya 2-2.

Christian Eriksen alifunga mabao yote ya Tottenham huku Che Adams naye akifunga mabao yote ya Shiffield.

Juzi Chelsea ilitinga fainali baada ya kupata ushindi wa jumla ya mabao 2-1 dhidi ya Liverpool.

Mchezo wa fainali utapigwa Machi mosi katika uwanja wa Wembely.

0 comments:

Post a Comment