Tuesday, 6 January 2015

Wajue wachezaji ambao hawana kasi duniani lakini wana madhara makubwa dimbani.

Ni wachezaji gani hapa duniani ambao wanacheza soka safi lakini si ya kasi zaidi?Siku zote tunawazungumzia  wachezaji wenye kasi zaidi lakini tumewasahau wanaocheza soka ambayo haina kasi lakini wana madhara makubwa sana wakiwa dimbani.
.

Wachezaji wasio na kasi dimbani kwa mujibu wa FIFA

Shirikisho la soka duniani (FIFA) limetoa orodha ya wachezaji ambao hawana kasi zaidi uwanjani lakini wana madhara makubwa sana pindi wakishika mpira.

FIFA limetoa orodha ya nyota 10 bora katika mwaka 2014

10. Francesco Totti – Roma.

Francesco Totti is one of the slowest soccer players in the world
Ni wachezaji wachache wanaoweza kudumu na klabu mmoja kwa sasa hapa duniani.lakini kwa muitaliano imekuwa tofauti,amedumu na Roma kwa muda wa miaka 23. Totti Hana kasi uwanjani lakini hawezi kukosekana katika first eleven ya Roma kutokana na uwezo wake wa kuwatengenezea wenzake nafasi ya kufunga mabao.

9. Emile Heskey –  Bolton Wanderers

Emile Heskey
Emile Heskey mchezaji wa zamani wa klabu ya  Liverpool amecheza mechi 150 akiwa na  Liverpool amecheza ndani ya  Leicester, Birmingham, Wigan na  Aston Villa akiwa katika ligi kuu ya Uingereza na amecheza mechi 62 akiwa na timu ya taifa ya England.kwa sasa ameniunga na

Bolton Wanderers baada ya kutangaza kurudi tena dimbani.



8. Andrea Pirlo – Juventus

Andrea Pirlo
Ingawa hana kasi dimbani, Andrea Pirlo anajulikana kama mmojawapo wa viungo bora dunian. Pirlo mwenye miaka  34 ni mchezaji wa tano kucheza mechi nyingi akiwa na timu ya taifa ya  Italia .Amecheza mechi 400 amebeba UEFA kwa upande wa vilabu mara mbili akiwa na AC Milan.

7. Gareth Barry – Everton

Gareth Barry
Gareth Barry ni mmojawapo kati ya nyota wenye spidi ndogo ligi kuu Uingereza,Barry ana uwezo mkubwa wa kucheza mpira na amecheza mechi 500akiwa na Aston Villa na Manchester City.

6. Peter Crouch – Stoke

Peter Crouch
Nyota huyu amecheza vilabu  12 mpaka sasa. Popote aendapo Peter Crouch Uwezo wake wa kucheza haubadiliki.

4. Carles Puyol – Amestaafu akiwa na Barcelona

Carles Puyol
Carles Puyol Ni baadhi ya mabeki bora duniani,kwa sasa ameachana na klabu yake ya Barcelona.

3. Per Mertesacker – Arsenal

Per Mertesacker
Per Mertesacker anacheza soka ambayo haina kasi katika ligi kuu Uingereza,lakini Per Mertesacker ameonesha uwezo wa hali ya juu msimu wa 2014/15,ametengeneza ukuta mzuri wa Arsenal akiwa na mlinzi mwenzake  Laurent Koscieln ingawa mwaka huu Mertesecker amekosa kombinasheni nzuri na mwenzake ambaye ameonekana kukumbwa na majeraha.

2. Daniel van Buyten – Bayern Munich

Daniel van Buyten
Daniel van Buyten akiwa katika Bundesliga,anahesabika kuwa ni mchezaji ambaye hana kasi ila ni mlinzi imara ndani ya klabu hiyo.

1. Brad Friedel – Tottenham Hotspur

 Brad Friedel
Kama kuna tuzo ya umri Brad Friedel  angestahili,kipa huyu ana miaka  43 kwa sasa ni kipa wa Tottenham ndiye mchezaji mwenye umri mkubwa katika ligi ya Uingereza lakini si mchezaji mwenye kasi sana , Brad Friedel amecheza mechi  310  akiwa na  Liverpool, Blackburn, Tottenham na ston Villa.

Imeandaliwa na Sports4lifeTz kwa msaada wa Tovuti ya FIFA.




 



0 comments:

Post a Comment