Monday, 30 June 2014

Huyu ndiye bingwa mpya wa mieleka mwaka 2014,awagaragaza wanaume 7,Randy aumizwa

Hatimaye jana (Juni 29)John Cena ametangazwa rasmi kuwa bingwa wa mieleka mwaka 2014 baada ya kuwagaragaza  wanaume 7 waliokuwa ulingoni kupambana katika mchezo wa  WWE Money in the Bank.
John Cena aliwashinda wanamieleka Kane,Roman Reigns, Randy Orton, Bray Wyatt, Bingwa wa Marekani  Sheamus, Cesaro na  Alberto Del Rio katika mchezo huo unaohusisha ngazi ili kumpata bingwa mpya wa uzito wa juu duniani.
Hapo kabla bingwa anayemiliki mkanda huo Daniel Bryan alijitoa rasmia  June 9 baada ya  kutopona vema na bado hajakamilisha matibabu yake.
Katika mchezo wa jana Orton alipigwa ngazi kichwani na kuchanika na kumfanya aumie vibaya lakini madakatari walimpa matibabu ambapo ameshonwa nyuzi kadhaa.







Money in the bank ni mchezo ambao wanamieleka hupigana na kisanduku  kufungwa  juu na kuning'inia na atakayeshinda ataweka ngazi ili atoe mkanda huo na ndipo atakuwa mshindi,na hivyo ndivyo alivyofanikiwa John Cena .
Kwenye historia  John Cena, Del Rio, Kane,Sheamus na Orton wamewahi kuchukua ubingwa huo wa dunia lakini  Reigns, Wyatt na  Cesaro hawajawahi kubeba ubingwa huo.
Matokeo mngine jana
Rusev  alishinda kwa Big EKikundi cha Stardust & Goldust kilishinda mbele ya RybAxelSeth Rollins amabaye alijitoa kutoka kikundi cha shield  aliwapiga  Dean Ambrose, Dolph Ziggler, Jack Swagger, Kofi Kingston na Rob Van Dam) na kushinda mkanda mwingine wa money in the bank kwa upande wa mkataba.

Adam Rose alishinda mbele ya  Damien SandowMabingwa kwenye kipengele ya timu ya muungano,mapacha Usos  walishinda mbele ya The Wyatt Family
Kwa mambo mengine yanmayojiri  usikose kufuatilia mtandao huu Sports4lifetz

0 comments:

Post a Comment