Sunday, 22 June 2014

Klose na Ronaldo wameweka rekodi zao mbele ya Ghana kila wakicheza,mhhhh pata uhondo zaidi.

Mchezaji  Miroslav Klose wa Ujerumani amesawazisha rekodi iliyokuwa inashikiliwa na nyota wa zamani wa Brazil  Ronaldo de Lima ya kufunga mabao 15 katika fainali za kombe la dunia baada ya kuingia akitokea benchi.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka  36 ambaye mwaka huu anacheza fainali zake za nne alifunga bao dakika ya  71 na ni bao lake la  69 katika mashindano ya kimataifa.
Klose  mfungaji bora wa kombe la dunia mwaka 2006    akiwa na mabao 5  alimaliza akiwa wa pili  mwaka  2002 akifunga mabao 5 pia na kule Afrika ya kusini mwaka 2010 alifunga mabao manne.List ya wachezaji waliofunga mabao mengi iko hapo chini.
Klose akiwatoka mabeki wa Ghana.
Sports4lifetz imebaaini kuwa Ronaldo aliweka rekodi ya kufunga mabao hayo 15 wakati Brazil ikicheza na Ghana katika fainali za kombe la dunia mwaka 2006 pia Klose amefunga bao lake la 15 mchezo dhidi ya Waafrika yaani Ghana.
Ni wazi kuwa Ronaldo na Klose wameweka rekodi zao mbele ya timu ya Afrika ambayo ni Ghana.






   Mchezaji/Nchi     Mabao   
Ronaldo-Brazil 15
Miroslav Klose-Ujerumani 15
Gerd Muller-Ujerumani 14 
 Just Fontaine-Ufaransa 13
 Pele-Brazil 12 
 Sandor Kocsis-Hungary 11 
 Jurgen Klinsmann-Ujerumani 11 
 Helmut Rahn-Ujerumani 10 
 Gary Lineker-uingereza 10 
 Gabriel Batistuta-Argentina 10 

0 comments:

Post a Comment