Gourcuff kocha mpya Algeria,mkataba kumalizika kombe la dunia 2018 Urusi.
Gourcuff alihusishwa sana kuchukua timu hiyo baada ya kombe la dunia ambapo viongozi wa shirikisho la soka la Algeria A.F.F wamethibitisha rasmi baada ya kikao cha jumamosi hii mjini Algiers.
Shirikisho hilo limesema kuwa kocha huyo mwenye miaka 59 ataanza kazi rasmi Agosti 1 mwaka huu.
Mkataba wake utamalizika baada ya kombe la dunia 2018 nchini Urusi.
Kwa mantiki hiyo kocha huyu atakuwepo mpaka mashindano ya Afrika mwaka 2015 na 2017.
Kwa mara ya mwisho Gourcuff alikuwa kocha wa klabu ya Lorient,ila aliachia ngazi mwezi mei mwaka huu,pia alishwahi kuwa kocha wa klabu ya Le Mans na Stade Rennes.
Ataanza kuiongoza Algeria mchezo dhidi ya Ethiopia mwezi septemba ili kufuzu AFCON 2015
Halilhodzic, ambaye aliacha kazi kwa sasa ni kocha wa Trabzonspor ya nchini Uturuki.

0 comments:
Post a Comment