Madrid mabingwa wa Super Cup,Ronaldo apiga mabao yote
Klabu ya Real Madrid imetwaa ubingwa wa Super Cup baada ya kupata ushindi wa 2-0 dhidi ya Sevilla, mchezo uliopigwa Uwanja wa Cardiff City mjini Cardiff na kutwaa.Mabao yote yalifungwa na Cristiano Ronaldo, huku bao la kwanza akifunga baada ya pasi ya nyota wa Wales, Gareth Bale Ronaldo alifunga bao la kwanza dakika ya 30.
Wakati bao la pili alifunga dakika ya 49 akipokea pasi ya Karim Benzema.
Baada ya mchezo kumalizika Ronaldo alisema kuwa Madrid itabeba ubingwa wa Hispania na pia kutetea taji lao la UEFA.
Huku kocha Carlo Ancelotti akimsifu kiungo wake mpya Toni Kroos kwa kuonesha kiwango kizuri hiyo jana.

0 comments:
Post a Comment