Tuesday, 26 August 2014

Mambo yameiva maombi AFCON 2017,Kenya wapeleka maombi,wasema wataandaa na Tanzania.

Kenya na Ethiopia  wametangaza  nia ya kuandaa michuano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika za Mwaka 2017, AFCON 2017, Baada ya  Shirikisho la Soka Africa kuwanyang’anya Libya Uenyeji.

CAF ilifuta Uenyaji wa Libya kutokana na Vita inayoendelea Nchini humo ambayo imesababisha kutojengwa kwa Viwanja vilivyoahidiwa kwa ajili ya Fainali hizo zinazoshirikisha Nchi 16

Taarifa kutoka nchini Kenya zimedai kuwa Shirikisho la soka nchini humo  imewaeleza CAF kuwa wataungana na Tanzania au Uganda au Rwanda kuandaa michuano hiyo.

Ikumbukwe kuwa jana Tanzania ilitangaza nia ya kuanaa michuano hiyo huku ikidai kuwa itapeleka taarifa kule Cairo,Misri.

Akizungumza na wanahabari jana jijini Dar es salaama,katibu mkuu wa TFF Selestine  Mwesigwa  alisema hatua hiyo inakuja baada ya kamati ya utendaji ya TFF kukutana mapema wikiendi iliyoipita.

TFF imetangaza nia ya kuwasilisha Maombi yake ya kuwa Mwenyeji wa AFCON 2017 na wamesema wataandaa Maombi hayo na kuyapeleka Serikalini ili kupata baraka za Viongozi wa Nchi kabla kupelekwa huko Cairo Makao Makuu ya CAF.

Ethiopia,walioanda michuano hiyo miaka ya  1962, 1968 na 1976,imesema itapeleka mara moja ombi hilo.
Rais wa shirikisho la soka la Ethiopia (EFF) Junedin Basha  amesma kuwa wana viwanja vizuri pale Addis Ababa na Bahir Dar na wanaendelea kutengeneza viwanja vingine.
 

0 comments:

Post a Comment