Thursday, 28 August 2014

Mshambuliaji Samuel Eto'o astaafu soka la kimataifa.

Mchezaji wa kimataifa wa Cameroon maarufu kama  Indomitable Lions ,Samuel Eto'o ametangaza kustaafu soka la kimataifa.
Mfungaji  huyo wa kihstoria nchini Cameroon ambaye amefunga mabao 56 ametangaza  kupitia mtandao wake wa instergram.

Eto'o aliyesajiliwa na  Everton juzi hatakwenda kushiriki michuano ya AFCON hapo mwakani na atabaki Uingereza kuitumikia klabu yake mpya.

Alisema kuwa  anahitimisha kuitumikia timu ya taifa na kuwashukuru watu wote wakiwamo mashabiki wa Afrika na dunia kwa ujumla kwa sapoti waliompatia.

Ikiumbukwe kuwa mapema wiki kocha wa timu ya taifa ya Cameroon  Volker Finke alitangaza kikosi chake kwa ajili ya kufuzu AFCON 2015 michezo dhidi ya  DR Congo hapo  September 6 na Ivory Coast  September 10 bila ya nahodha wake  Samuel Eto’o.

Wachezaji wengine waliotemwa ni Aurelien Chedjou, Benoit Assou-Ekotto, Jean II Makoun, Achille Webo na  Charles Itandje wakati mchezaji wa  Barcelona Alexandre Song anatumikia adhabu ya michezo mitatu baada ya kufanya makosa kombe la dunia  2014 kule nchini Brazil.

Nyota huyo wa zamani wa  Barcelona, Inter na  Real Madrid alianza kuitumikia nchi mwaka 1997  na walifungwa mabao 5-0 na  Costa Rica.
Mchezo wa mwisho ndani ya kikosi cha Indomitable Lions ni dhidi ya  Mexico  katika fainali za kombe la dunia,

0 comments:

Post a Comment