Valverde amsubiri kwa hamu Dembele


Kocha mkuu  wa Barcelona Ernesto Valverde amesema kuwa Ousmane Dembele ataleta mafanikio ndani ya klabu yake.

Jana  mchana kuwa Barcelona walikuwa wameshafikia makubaliano ya dili la paundi milioni 96.8 na Borussia Dortmund kwa ajili ya uhamisho wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, ambaye amekuwa mchezaji ghali zaidi wa pili duniani.

Mshambuliaji huyo amefunga mara 10 na kutoa pasi za mabao 18 katika mechi 47 alizocheza Dortmund msimu wa 2016-17, na Valverde amebainisha kuwa uzalendo unamshinda kuendelea kusubiri mchezaji huyo kutua Camp Nou.
 

Barcelona wataendelea na kampeni za La Liga 2017-18 kucheza dhidi ya Alaves Jumamosi usiku.

Ousmane Dembele anatarajiwa kutua Barcelona Jumapili na Jumatatu atafanyiwa vipimo kabla ya kusaini mkataba wa miaka mitano Camp Nou.



Read More

VPL 2017/18 kuanza leo

Ligi kuu soka TANZANIA BARA kwa msimu wa 2017/18 Itaanza kutimua vumbi leo katika viwanja saba tofauti hapa nchini.

Mabingwa wa ngao ya jamii na michuano ya kombe la shirikisho SIMBA wataanza kutupa karata yao ya kwanza kupambana na RUVU SHOOTING,uwanja wa taifa DAR ES SALAAM.

Mbao watakuwa wageni wa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya Majimaji ya Songea itakayosafiri hadi Mbeya kucheza na Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine jijini humo huku Njombe Mji ikiialika Tanzania Prisons ya Mbeya kwenye Uwanja wa Sabasaba huko Makambako.

Kadhalika Uwanja wa Manungu ulioko Turiani, Mtibwa mkoani Morogoro, Mtibwa Sugar itaikaribisha Stand United ya Shinyanga kwenye mchezo mwingine wa VPL ilihali Azam atakuwa mgeni wa Ndanda FC kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mwadui watakuwa wenyeji wa Singida United ya Singida kwenye Uwanja wa Mwadui huko Shinyanga na Jumapili kutakuwa na Mchezo mmoja utakaokutanisha Young Africans na Lipuli kwenye Uwanja wa Uhuru jijini
Wakati  huohuo  shirikisho la soka nchini Tanzania- TFF imesema Ni msimu mpya utakaotoa timu bingwa mpya itakayoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika inayoandaliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), msimu wa 2019.

Itakumbukwa, msimu wa CAF wa 2018, timu itakayoiwakilisha nchi ni Young Africans SC ambayo ni Bingwa wa VPL msimu 2016/17 wakati michuano ya Kombe la Shirikisho, Tanzania itawakilishwa na Simba SC.

TFF inazitakia kila la kheri timu zote zinazoshiriki ligi hii, ikiamini kwamba uadilifu utaongoza mbele ya taratibu, kanuni na sheria zinazosimamia mpira wa miguu hapa nchini na kwingineko.
Read More

Ingia hapa kuona msimamo wa EPL,leo Bingwa mtetezi anacheza na Crystal Palace.

Ligi kuu ya Uingereza imeendelea kunguruma juzi na jana kwa timu zinazoshikilia nafasi nne za juu kushinda isipokuwa Manchester City ambao hawajacheza.

City watacheza leo usiku dhidi ya Crystal Palace.

Klabu hiyo inahitaji ushindi ili kurudi katika nafasi ya pili na ikitokea wakapoteza mchezo huo wataendelea kushikilia nafasi ya nne baada ya Arsenal na Manchster United kushika nafasi ya pili na tatu.

MSIMAMO
PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Chelsea30217263263770
2Arsenal31196662323063
3Manchester United31188555282762
4Manchester City30187562283461
5Liverpool3116694536954
6Tottenham Hotspur3116695045554
7Southampton311651042222053
8Swansea City31137113739-246
9West Ham United31119114139242
10Stoke City31126133539-442
11Everton31910123942-337
12Crystal Palace3099123641-536
13Newcastle United3198143349-1635
14West Bromwich Albion3189142843-1533
15Sunderland31514122444-2029
16Hull City31610152943-1428
17Aston Villa3177172042-2228
18Burnley31511152649-2326
19Queens Park Rangers3174203555-2025
20Leicester City3057182949-2022




Read More

VPL Mtibwa yasukumwa na Stendi hadi mstari wa kushuka daraja.

Klabu ya Stand United ya Shinyanga imefanikiwa kushinda bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Mtibwa Sugar iliyochezwa kwa siku mbili kuanzia hapo jana na leo.

Bao la Stand United lilifungwa jana na Haruna Chonongo katika dakika ya 12 kabla ya pambano hilo kuvunjika dakika ya 33 kufuatia mvua kubwa kunyesha mjini Shinyanga.

Mchezo huo ulichezeshwa kwa dakika 57 zilizosalia asubuhi na mechi kumalizika kwa 0-0.

Kwa matokeo hayo Stand United wanafikisha alama 24, alama moja mbele ya Mtibwa wenye alama 23 na kuwafanya Mtibwa kushikilia nafasi ya 12 kati ya timu 14 zinazoshiriki ligi ya VPL.

Ligi hiyo itaendelea kunguruma jioni kwa mchezo moja kupigwa uwanja huo wa Kambarage ambapo wenyeji Kagera Suukari wanachuana na Simba SC.

Awali mechi hiyo ilitakiwa kupigwa jumamosi iliyopita, lakini iliahirishwa kutokana na uwanja kujaa maji kutokana na mvula zinazoendelea kunyesha.
Read More

Ratiba ya EPL kesho,patashika kubwa ni Arsenal na Liverpool

Ligi kuu nchini Uingereza itaendelea kunguruma kesho kwa viwanja  saba kuwaka moto.

Washika bunduki Arsenal watawaalika  Liverpool  huku Everton wakipepetana na  Southampton ,mashetani wekundu Manchester  United watakwaruzana na Aston Villa,Swansea watakabana koo na  Hull,kadhalika vinara Chelsea watatwangana na  Stoke  city.

Ratiba Jumamosi,muda ni kwa saa za TANZANIA.

ArsenalvLiverpoolEmirates Stadium14:45

West Bromwich AlbionvQueens Park RangersThe Hawthorns17:00

Swansea CityvHull CityLiberty Stadium17:00 
Manchester UnitedvAston VillaOld Trafford17:00

Leicester CityvWest Ham UnitedKing Power Stadium17:00 
EvertonvSouthamptonGoodison Park17:00 
ChelseavStoke CityStamford Bridge19:30














Read More

VPL kunguruma kesho,Kagera sugar kuwaalika Simba,Coast na Prisons

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara  itaendelea kunguruma kesho na keshokutwa   katika viwanja sita nchini, kwa michezo minne kuchezwa siku ya jumamosi na michezo mwiwili kuchezwa siku ya jumapili.

Jumamosi uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, Kagera Sugar watakuwa wenyeji wa Simba SC kutoka jijini Dar es salaam, huku jijini Tanga Coastal Union wakiwakaribisha maafande wa jeshi la Magereza nchini Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Mkwakwani.

Ndanda FC ya Mtwara watakuwa wenyeji wa wagonga nyundo timu ya Mbeya City katika uwanja wa Nagwanda Sijaona, wakati maafande wa Jeshi la Kujenga Taifa Ruvu Shooting wakicheza na ndugu zao JKT Ruvu katika uwanja wa Mabatin uliopo Mlandizi.

Siku ya jumapili Stand United watawakaribisha wakata miwa kutoka Morogoro Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Kambarage, huku Mgambo Shooting wakiwa wenyeji wa timu ya  Polisi Morogoro kwenye uwanja wa Mkwakani jijini Tanga.
Read More

Kocha bora wa mwezi EPL kuna Wenger,Van Gaal,Sherwood na Koeman.

Kocha wa klabu ya Manchester United mholanzi  Louis van Gaal ametajwa kuwania tuzo za kocha bora wa mwezi katika ligi kuu Uingereza.

Katika mwezi Machi klabu ya Manchestert United imekusanya alama tisa katika mechi muhimu,mechi hizo ni  ya  Tottenham Katika dimba la  Old Trafford na Liverpool katika uwanja wa Anfield.

Timu hiyo inashikilia nafasi ya nne katika msimamo.
.
Makocha wengine waliotajwa ni pamoja na  Arsene Wenger wa Arsenal , Tim Sherwood wa Aston Villa na Ronald Koeman. Southampton.

Washika bunduki Arsenal wameshinda mechi zao zote nne ndani ya mwezi Machi na kushikilia nafasi ya tatu nyuma ya Manchester City.

Sherwood alianza kibarua ndani ya Villa Park baada ya  Paul Lambert kutimuliwa amekusanya alama sita na kuiondoa Villa katika mstari wa kushuka daraja.

Koeman, ameipa Southampton alama 7 katika mechi tatu sambamba na sare dhidi ya vinara Chelsea Uwanja wa  Stamford Bridge.

Mshindi atatangazwa kesho.
Read More

Michuano ya Miami Open yafikia nusu fainali.

Mcheza tenis wa Uingereza Andy Murray amefanikiwa kuingia nusu fainali baada ya kumshinda Dominic Thiem raia wa Austria katika mashindano ya Miami Open yanayoendelea huko nchini Marekani.

Pamoja na kupoteza seti ya kwanza ya mchezo huo,Murray alifanikiwa kuzinduka na kushinda kwa jumla ya seti 3-6 6-4 na 6-1.

Murray mwenye umri wa miaka 27, anaweza kupambana na Tomas Berdych raia wa Czech ama Muajentina Juan Monaco katika nusu fainali ya mashindano hayo.

Naye Serena Williams amepata ushindi wa 700 tangu aanze kucheza mchezo huo baada ya kuingia nusu fainali kwa kumbwaga mjerumani Sabine Lisicki.
Chanzo BBC.
Read More

Kanu asema Supe Eagles si wazuri kwa sasa.


Nyota wa zamani wa klabu ya  Arsenal na timu ya taifa ya Nigeria  Kanu Nwankwo amesisitiza kuwa timu ya taifa ya Nigeria si nzuri ila amesema itakuja kuwa nzuri muda si mrefu.

Nigeria maarufu kwa jina la Super Eagles haipati matokeo mazuri  tokea watwae ubingwa wa Afrika mwaka 2013.

Kanu amesema kuwa kushindwa kufuzu mashindano ya AFCON mwaka 2015 kule Equatorial Guinea si picha nzuri ila anaamini kuwa timu itakuwa nzuri siki zijazo.

Nyota huyo aliyewahi kuzichezea pia  Ajax na  Inter Milan ameongeza kuwa mgogoro wa soka nchini kwao lazima uwekwe wazi ili timu ipate matokeo mazuri.


Kanu  aliyechezea Nigeria mechi  87 tokea  1994 hadi  2011 ameongeza kuwa hafurahishwi na  mgogoro unaoendelea nchini mwake.
Read More